General

Name
Muhidin Issa Michuzi
Region
Dar es Salaam

News

Kwi kwi kwenye libeneke la blogu ya Issa Michuzi linatatuliwa
16 years ago
nachukua nafasi hii kutoa asante kwa mh. kunitembelea na wakati huo huo kutoa ufafanuzi na kuomba radhi wadau wote kwa kwikwi iliyotuandama juma zima. ni kwamba, katika juhudi za kufanya globu ya jamii iwe bora zaidi, tumepata server ambayo ina nafasi kubwa hata za kuanzisha libeneke la video kama tulivyoahidi awali. tatizo linakuja kwamba mitambo ya host wetu inakuwa ikiteleza mara kwa mara kudaka link ya globu ya jamii na kusababisha kwikwi ya mara kwa mara. na ili kukomesha kwikwi hiyo imeonekana bora tuendeleze libeneke kwenye anuani ya issamichuzi.blogspot.com kama ilivyokuwa zamani wakati tukisubiri wahandisi wa host wetu arekebishe mambo. kunradhi kwa usumbufu unaowapata wadau na nashukuru kwa jinsi maelfu ya wadau wanavyolifuatilia swala hili na kunipa moyo kuwa nisikate tamaa. nami naahidi kuendeleza libeneke bila kusita pamoja na kukumbwa na changamoto za kiufundi ambazo ziko nje ya uwezo wetu. natumai mtaendelea kutuelewa na kutuvumilia Source: issamichuzi.blogspot.com
Mdau Michuzi awa Mkuu wa Wilaya ya Tegeta
Mdau Michuzi awa Mkuu wa Wilaya ya Tegeta
17 years ago
RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE LEO AMEMTEUA NDUGU MUHIDIN ISSA MICHUZI KUWA MKUU MPYA WA WILAYA MPYA YA TEGETA ILIYOPO WILAYA YA ILALA, DAR ES SALAAM. TAARIFA TOKA IKULU IMESEMA UTEUZI HUO, AMBAO UNAANZA MARA MOJA, UNAKUJA SIKU MOJA TU BAADA YA SERIKALI KURIDHIA OMBI LA WAKAZI WA TEGETA KUIFANYA SEHEMU HIYO KUBWA KUWA WILAYA KAMILI, NA KUFANYA DAR ES SALAAM KUWA NA WILAYA NNE - ZIKIWEMO ILALA, TEMEKE NA KINONDONI. KABLA YA UTEUZI HUO, NDUGU MICHUZI ALIKUWA NI MPIGA PICHA MWANDAMIZI WA MAGAZETI YA SERIKALI YA DAILY NEWS NA HABARI LEO, KAZI AMBAYO IMEBIDI AIAGE ILI KUSHIKA WADHIFA WAKE HUO MPYA. "HAKIKA NIMEHEMEWA KWANI KAZI YA UKUU WA WILAYA SI NDOGO UKIZINGATIA KWAMBA NDIYO SHINA LA SERIKALI KUU" NDUGU MICHUZI ALISEMA BAADA YA KUHOJIWA NA GAZETI HILI LEO JIONI. HII SI MARA YA KWANZA KWA RAIS KIKWETE KUTEUA WANAHABARI KUSHIKA NYADHIFA KAMA HIYO, WENGINE WAKIWA NI MH. BETTY MKWASA AMBAYE NI MKUU WA WILAYA YA KOROGWE, NA MH, HALIMA KIHEMBA, MKUU WA WILAYA YA KILOSA. WOTE HAWA NI WANAHABARI AKIONGELEA HATMA YA BLOGU YAKE, MH. MICHUZI AMESEMA KWA LUGHA YAKE ANAYOPENDA KUITUMIA KWAMBA ATAENDELEZA LIBENEKE KAMA KAWAIDA HATA KAMA ANGECHAGULIWA KUWA RAIS. "HII BLOGU NI YA JAMII HIVYO SINTOELEWEKA ENDAPO KAMA NITAAMUA KUIACHA ATI KWA SABABU YA KUPATA WADHIFA SERIKALINI. "SIONI NI JINSI GANI NITASHINDWA KUTEKELEZA MAJUKUMU YANGU KAMA MKUU WA WILAYA MPYA YA TEGETA NA WAKATI HUO HUO KUHUDUMIA JAMII KUPITIA BLOGU YAO HII," ALISEMA MH. MICHUZI. UAMUZI WA KUIFANYA TEGETA KUWA WILAYA KAMILI UMEFIKIWA BAADA YA KUONEKANA KWAMBA ENEO HILO LILILOPO KASKAZINI MWA JIJI LA DAR ES SALAAM LIMEKUA KWA KASI NA KUWA NA WAKAZI WENGI KIASI YA KWAMBA KUENDELEA KUWA CHINI YA WILAYA INGINE KUNGELETA MATATIZO KWA WAKAZI WAKE. MH. MICHUZI ANATARAJIWA KUAPISHWA LEO ASUBUHI NA MKUU WA MKOA WA DAR ES SALAAM, MH ABBAS KANDORO, KATIKA SHEREHE ZILIZOPANGWA KUFANYIKA KWENYE OFISI ZA MKUU HUYO WA MKOA, ILALA BOMANI. SOURCE: ISSAMICHUZI.BLOGSPOT.COM

Contacts

  • http://issamichuzi.blogspot.com

Pictures

Comments

Drafti

Chemsha bongo Uswahili

Hebu tuone utalaam wako

Cheza hapa