Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limepokea barua kutoka uongozi wa Simba ikielezea kutotambua mkutano ulioandaliwa na wanaodaiwa kuwa wanachama wake na kufanyika jana ukumbi wa Starlight, Dar es Salaam.
Vilevile katika barua hiyo uongozi wa Simba umeahidi kuitisha mkutano wa wanachama wake. Mkutano huo utaitishwa na Mwenyekiti wa Simba kwa mujibu wa katiba ya klabu hiyo.
Kutokana na hali hiyo, TFF imeitisha mara moja kikao cha Kamati ya Sheria, Maadili na Hadhi za Wachezaji kinachoongozwa na Wakili Alex Mgongolwa kwa ajili ya kutoa mwongozo kwa matukio ya aina hiyo.
Hata hivyo, TFF tunasisitiza kwa wanachama wetu ikiwemo Simba kuwa wanachama wanapotaka kufanya uamuzi wowote ule wanatakiwa kuzingatia katiba na kanuni zilizopo.
Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)
Napata shida sana na mwenendo wetu wa uendeshaji wa michezo nchini. Migogoro imekua sehemu ya vilabu vyetu, na kwa hali hii tusitaraji maendeleo ya mpira wa miguu katika nchi yetu. Je TFF mnatoa elimu ya uongozi katika kuendesha michezo Kwenye ngazi ya vilabu? Nakama mnaendesha elimu hiyo nikwamuda gani? Mana ninyi kama chombo chenye dhamana hamuwezi mkataraji mchezo huo kukua kama hamkuwatengenezea msingi
ReplyDeleteTFF saidieni kuzuia migogoro kwenye vilabu, michezo imepoteza dira Tanzania
ReplyDelete