Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) akipokea Nakala za Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi Mteule wa Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) hapa nchini, Mhe. Abdulla Ibrahim Al Suwaidi. Hafla hiyo fupi ilifanyika Ofisi kwa Mhe. Waziri Membe leo tarehe 14 Machi, 2013.
Mhe. Membe akizungumza na Mhe. Balozi Al Suwaidi  masuala mbalimbali ya ushirikiano kati ya Tanzania na UAE mara baada ya kupokea Nakala za Hati za Utambulisho za Balozi huyo.
Mhe. Balozi Al Suwaidi akichangia hoja wakati wa mazungumzo yake na Mhe. Membe. Mwingine katika picha ni Bw. Hangi Mgaka, Afisa Mambo ya Nje katika Idara ya Mashariki ya Kati.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Ama kweli Masheikh wetu wa Uarabuni neema kila siku wanayo.

    Haya mavazi kama alivyovaa Mhe.Balozi wa UAE hapa Bongo Tambarale mtu anavaa siku ya Harusi pekee tena kwa Mipango!

    Usikute mtu siku ya Harusi yake mipango inafanywa Joho linaazimwa kwa Imam wa Masjid hapo jirani?

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...