Rais wa TALISS Swimming Club Bi. Najat Saleh Ahmed (mwenye miwani nyeusi) akizungumza na washiriki pamoja na wageni waalikwa wakati wa ufunguzi wa mashindano ya kuogelea yaliyoshirikisha Club mbalimbali na kwa rika tofauti yaliyodhaminiwa na Kampuni ya CFAO Motors wauzaji wa magari ya kisasa hapa nchini yaliyofanyika katika bwawa la kuogelea la shule ya Kimataifa ya Tanganyika (IST).
Amesema Mashindano hayo hufanyika kila mwaka na kushirikisha vilabu na watu binafsi wenye ujuzi wa kuogelea unaofikia kiwango cha kushiriki mashindano.
Aidha Bi. Najat Ahmed ameomba wadau zaidi kujitokeza kudhamini mashindano hayo na kuiomba Serikali ijitokeze na kujenga mabwawa yanayohitajika kwa ajili ya watu kujifunza kuogelea ili kuweza kujiokoa katika ajali za majini.
Pichani juu na chini washiriki wa club mbalimbali za kuogelea wakipita mbele wazazi na makocha kwa ajili ya utambulisho.
Official wakijipanga tayari kuanza mashindano hayo yaliyohusisha Clubs mbalimbali kutoka sehemu tofauti.
Pichani juu na chini ni washiriki wajitosa kwenye bwawa hilo kuchuana katika mashindano ya kuogelea yaliyoratibiwa na TALISS Swim Club na kudhaminiwa na kampuni ya CFAO Motors ya jijini Dar.
Picha juu na chini Sehemu ya watazamaji wakishuhudia mashindano hayo yaliyofanyika mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam katika shule ya Kimataifa ya Tanganyika (IST).
Picha juu na chini Meneja Masoko wa CFAO Motors Tharaia Ahmed akiwavalisha medali washindi wa mashindano hayo katika kategori mbalimbali. CFAO Motors imeamua kudhamini mashindano hayo baada ya kuona umuhimu wa vijana kujua kuogelea ili kuweza kujiokoa katika majanga yanayohusiha ajali za majini zinazopelekea vifo vya watoto ikiwa ndio lengo la TALISS.
Rais wa TALISS Swimming Club Bi. Najat Saleh Ahmed akikabidhi medali kwa mmoja wa washindi wa mashindano hayo yaliyodhaminiwa na Kampuni ya CFAO Motors.
Picha juu na chini ni Mkurugenzi wa Biashara wa Kampuni ya CFAO Motors Wayne Mcintosh ambaye pia alikuwa MC katika mashindano hayo akikabidhi vikombe kwa washindi wa jumla walioshiriki TALISS Swimming Championships 2013.
Umati wa watu wakiwemo wazazi, ndugu na jamaa pamoja makocha waliohudhuria kushuhudia mashindano ya kuogelea ya TALISS yaliyohusisha vilabu kutoka sehemu mbalimbali.
Baadhi ya wageni waliohudhuria kutazama mashindano ya kuogelea katika shule ya Kimataifa ya Tanganyika (IST) wakikagua gari mpya aina ya Nissan Y62 inayosambazwa na Kampuni ya CFAO Motors.
The extinction of mpingo.
ReplyDeleteWapi naweza kupata contacts za swimming club za Dar? Nataka nirudi kuni kiwango changu! Mdau
ReplyDeleteHilo ndilo tatizo letu sisi...Siku zote malengo ndio yanayodetermine uhai wa career yako hapo baadae..Malengo yetu katika football ni kuwashughulisha vijana ili waachane na makundi ya kuvuta bange,na sasa hapa katika kuogelea tunasema lengo ni kuwafundisha watoto wajue kujiokoa pale vyombo vya majini vinapozama na lengo sio kuwa fanya wawe mabalozi wetu wazuri katika olympiki kama akina MICHAEL PHELPS..Basi inabidi TALLIS waanzishe na mafunzo ya kudaivu katika BARABARA YA LAMI ili tuweze kuwa na sugu zakutosha pale ajali ya barabarani(ambazo ndizo nyingi kuliko za majini)zitakapotokea tusipate madhara....
ReplyDeleteMon Feb 25, 11:25:00 am 2013
ReplyDeleteAnonymous said...
Sasa ni hivi TALISS leongo lao pia ni hilo sio tu ajali za majini bali mwandishi aliteleza na kushindwa kuliweka sawa swala la Olympic.
Nashukuru hilo nalo neno kosa sio la TALISS ni la mwandishi.
Pongezi mchangiaji wa mwanzo "the extinction of mpingo" hili ni la kutafakari kwa undani, tukiendelea na kudharau ndio hilo litatokea ama amani itatoweka hapo mbeleni kwani mpingo nao huenda ukatoa mbegu sugu na zikaamua kujihimili "Mpingo fights back". Kwa taswira ya picha tu basi mimi ningesema hii ni South Africa, Holland, U.S.A ama U.K. Lazima kuwe na mipango maalumu ya kulazimisha sehemu zote za huduma ziwafikie na wazawa hata kama ni kwa kuweka fungu la hizi sehemu ziende kwa watu wanaoishi sehemu hizo kwa bei nafuu itayopangwa na serekali za mitaa za sehemu hizo ili kuepuka ubaguzi kwa kutumia kipato.
ReplyDeleteMdau wa Kwanza na wa Tano hapo juu,
ReplyDeleteNi sawa anaposema 'extinction of Mpingo' lakini tukirudi nyuma ni kuwa tunapoona mtoto wa Kihindi anatumia Swimming Pool ni kuwa wazazi wake wamelipia gharama hizo ingawa ni kubwa kidogo.
Tatizo letu sisi akina Maganga Bin Mpingo wapo wenye uwezo wa kama wazazi wa hao watoto wahindi hapo lakini mara zote Kiama chetu akina Maganga Mpingo hela nyingi tunaelekeza Bar na Pub badala ya huduma za watoto na malezi ikiwemo burudani zao.
Tukija upande wa Serikali za Mitaa, ni kuwa Wahindi wanaweka mipango ktk Society zao wanatoa au wanachangia gharama za sehemu za recreation au burudani mfano Swimming club nyingi ni zao kwa kuwa wanazingatia gharama hizo, wakati serikali zetu za Mitaa ni butu ile hata kuzibua mifereji wanangoja Serikali ifanye au itokee NGO au Mengi mdhamini afanye!
Mdau wa kwanza anony Mon Feb 25, 11:18:00 am 2013
ReplyDelete'extinction of mpingo'
Wazazi wa kikonongo tunaelekeza fedha nyingi kama mababa tunaelekeza fungu kubwa nyumba ndogo badala ya burudani kama kuogelea na michezo kwa watoto!