Oktoba 12,2013 NMB ilizindua promosheni ya Ki-COLLEGE Plus na NMB inayowawezesha wanafunzi wa elimu ya juu wenye akaunti na NMB Student Account kupata nafasi ya kuingia kwenye droo na kujishindia zawadi mbalimbali kama: simu za mkononi aina ya ‘Samsung Galaxy Pocket Plus 3g’ na kujishindia fulana za NMB.
Zaidi ya washindi 400 waliofungua NMB Student Account,walioweka amana katika akaunti zao au kujiunga na NMB mobile wameweza kuingia kwenye droo na wamepata nafasi ya kujishindia zawadi kwenye promosheni ya Ki-COLLEGE Plus iliyodumu kwa miezi mitatu.
Katika droo ya mwisho iliyochezwa jana, jumla ya washindi 40 wamepata bahati ya kujishindia simu za mkononi aina ya ‘Samsung Galaxy Pocket Plus 3g’ na washindi wengine 100 kujishindia fulana za NMB.
Mkuu wa kitengo cha Biashara NMB (tatu kushoto) Filbert Mponzi akibonyeza kitufe ili kuwapata washindi wa droo ya mwisho ya Ki-COLLEGE Plus na NMB ambapo washindi 140 wamejishindia zawadi mbali mbali kama vile simu ya mkononi aina ya ‘Samsung Galaxy Pocket Plus 3g’ na kujishindia fulana za NMB. Kwanza kushoto ni Meneja Masoko wa NMB, Yusuf Shenyagwa , Meneja wa Amana za Wateja wa NMB, Boma Raballa, Meneja Huduma kampuni ya Selcom, Everline Simpilu selcom na Mkaguzi kutoka Bodi ya Michezo ya Kubahatisha, Mrisho Millao.
Mkuu wa Idara ya Biashara wa NMB, Filbert Mponzi ( kwanza kulia), Meneja wa Amana za Wateja wa NMB, Boma Raballa na Meneja wa Masoko wa NMB , Yusuf Shenyagwa wakionyesha sehemu ya zawadi mbali mbali ambazo washindi 140 wa kampeni ya Ki-college plus na NMB watakabidhiwa katika promosheni iliyodumu kwa miezi mitatu. Katika droo ya mwisho iliyofanyika jana, jumla ya washindi 140 wamepatikana.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...