Sign in to confirm you’re not a bot
This helps protect our community. Learn more
SERIKALI YAKIRI KUWEPO UPUNGUFU WA WALIMU MASOMO YA SAYANSI
4Likes
365Views
May 292025
Serikali imethibitisha kuwepo kwa upungufu mkubwa wa walimu wa masomo ya sayansi na hisabati katika shule za msingi na sekondari nchini, hali inayohatarisha maendeleo ya kitaaluma ya wanafunzi katika maeneo mengi. Akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalumu, Shally Raymond, leo Alhamisi Mei 29, 2025 bungeni jijini Dodoma, Naibu Waziri wa Ofisi ya Rais – Tamisemi, Zainabu Katimba amesema: “Mahitaji ya walimu wa masomo ya sayansi na hisabati ni 47,354, waliopo ni 30,042 hivyo kuna upungufu wa walimu 17,312,”. Kwa upande wa shule za msingi, Katimba amesema mahitaji ya walimu ni 298,687, huku waliopo wakiwa ni 173,861, hivyo kuwepo na upungufu wa walimu 124,826. Amesema Serikali inaendelea kufuatilia hali hiyo kwa karibu na itaendelea kuajiri walimu, wakiwemo wa masomo ya sayansi, kadri bajeti ya fedha inavyoruhusu. “Serikali inafahamu changamoto hii, na hatua ya ongezeko la wanafunzi kutokana na utekelezaji wa sera ya elimu bila malipo imechangia kuongezeka kwa mahitaji ya walimu,” ameeleza Katimba.

Mwananchi Digital

1.15M subscribers