Sign in to confirm you’re not a bot
This helps protect our community. Learn more
Mbunge akerwa na wanafunzi kusimama mwaka mzima katika mabasi
Mbunge wa Viti Maalumu, Latifa Juakali, amesema baadhi ya wanafunzi wa shule za msingi hupanda mabasi ya shule bila nafasi ya kuketi kwa mwaka mzima, hali inayowaathiri kimaendeleo na kimaadili. Akizungumza bungeni leo, Alhamisi Mei 22, 2025, Latifa ameitaka Serikali kutoa kauli kuhusu shule zinazokiuka haki hiyo na kupendekeza kuwepo kwa wasimamizi wa kike na kiume ndani ya mabasi ya shule. Pia amehoji haja ya kuwepo kwa walimu wa maadili mashuleni. Akijibu, Naibu Waziri wa Ofisi ya Rais-Tamisemi, Zainab Katimba amesema Serikali imeshaelekeza kuwepo kwa wasimamizi wa jinsia zote katika mabasi ili kuhakikisha usalama wa watoto. Amesisitiza kuwa Serikali inaendelea kutoa mafunzo kwa walimu na wadau wengine kuhusu ulinzi wa wanafunzi. Ametaja kampeni dhidi ya ukatili wa kijinsia, mafunzo kwa walimu wa ushauri na unasihi, na viongozi wa shule kuwa sehemu ya mikakati ya kulinda wanafunzi.

Mwananchi Digital

1.15M subscribers
Chat Replay is disabled for this Premiere.