Mmoja kati ya Wakulima wa Kijiji cha Nguruweni Dole Mzee Kitwana
Mustaha aliishukuru na Kuipongeza
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kupitia Makamu wa Pili wa Rais wa
Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi kwa
kukamilisha ahadi yake ya kuwapatia hati za umiliki wa mashamba wakulima hao kwa ajili ya kilimo katika
maeneo yaliyowahi kuleta mgogoro kwa muda mrefu.
Baadhi ya wananchi na wakulima wa Kijiji cha Nguruweni wakiwa katika
mkutano maalum uliotishwa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi
Seif wa kukabidhiwa hati za umiliki wa mashamba ya kilimo katika maeneo yao.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif akizungumza na
wakulima wa Kijiji cha Nguruweni kabla ya kuwakabidhi hati za umiliki wa
mashamba ya kilimo wakulima hao.
Balozi Seif Ali Iddi akimkabidhi Hati ya umiliki wa shamba Bibi
Josephine Yohana kwenye hafla maalum ya kumaliza mgogoro wa mashamba katika
kijiji hicho.
Balozi Seif akimpatia Hati Bwana Mohd Ali Pili ya kumiliki eneo la
kilimo katika Kijiji cha Nguruweni
ambako kuliibuka mgogoro uliosababishwa na kuinbgizwa watu wasiohusika
na maeneo hayo kwa kilimo. Picha na
Hassan Issa wa – OMPR – ZNZ.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...