MFUKO wa vyombo vya habari nchini TMF umefanya ziara ya kutembelea katika kijiji cha Chekereni kilichopo wilaya ya Moshi vijijini kujionea hali ya uchafuzi wa maji katika mto Karanga yanayodaiwa kuwaathili wakazi wa maeneo hayo.

Afisa tathimini na ufuatiliaji wa mfuko wa vyombo vya habari nchini TMF Sanne van den Berg alifika katika maeneo mbalimbali ya mto huo kujionea hali hali hali ikiwa ni pamoja na kuzungumza na wakazi wa maeneo hayo wakiwemo viongozi wa kijiji.

Hatua hiyo imefuatia kutolewa taarifa za uchafuzi wa maji katika mto huo unaofanywa na baadhi ya viwanda vilivyoko jirani na mto huo na kusababisha madhara kwa wakazi wa vijiji vilivyoko kando ya mto huo.
Afisa tathimini na ufuatiliaji wa mfuko wa vyombo vya habari nchini TMF Sanne van den Berg akiongea na mmoja wa wakazi wa kijiji cha Chekereni alipotembelea mto Karanga kujionea uchafuzi unaofanyika.
Sehemu ya mto Karanga iliyomeguka ikiwa jirani kabisa na nyumba zilizojengwa kando ya mto huo.
Sehemu ya kuhifadhia maji machafu kabla ya kuelekezwa mto Karanga,maji yanayotoka kiwanda cha karatasi cha Kibo ambayo hata hivyo sehemu hiyo inaonekna haitumiki .
Afisa tathimini na ufuatiliaji wa mfuko wa vyombo vya habari nchini TMF Sanne van den Berg akipita katika daraja lililopo jirani kabisa na eneo kunako fanyika uchafuzi wa maji .
Sehemu ambayo uchafuzi wa maji ya mto Karanga kama inavyoonekana .
Afisa tathimini na ufuatiliaji wa mfuko wa vyombo vya habari nchini TMF Sanne van den Berg akiongea na mwenyekiti wa kitongoji cha Relini Sadick Kubingwa alipomtembelea nyumbani kwake kuzungumza naye kuhusu uchafuzi wa maji mto Karanga. Picha na Dixon Busagaga wa globu ya jamii Moshi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...