Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo akimshukuru Bw. R. de Roon, mmoja wa wabunge wa Bunge la Uholanzi waliofika Ofisi za Wizara ya Nishati na Madini kwa ajili ya kupata ufahamu zaidi kuhusu sekta ndogo ya gesi na mafuta.
Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo akiwa katika picha ya pamoja na Balozi mteule wa Uholanzi nchini Tanzania Mhe.Jaap Frederiks (kulia) pamoja na Bw. R. de Roon (Mb.) mara walipomtembelea ofisini kwake.
Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo akiwa pamoja na ujumbe kutoka Uholanzi ulioongozwa na Balozi mteule wa Uholanzi nchini Tanzania Mhe.Jaap Frederiks (wa tatu kutoka kulia) pamoja na wabunge wa Bunge la Uholanzi wakati walipomtembelea ofisini kwake.
Balozi mteule wa Uholanzi hapa nchini, Mhe.Jaap Frederiks akiongozana na ujumbe wa wabunge 7 kutoka Bunge la Uholanzi wamemtembelea Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo kwa nia ya kupata ufahamu zaidi kuhusu masuala mbalimbali yanayohusu sekta ndogo ya mafuta na gesi nchini.
Akiongea katika mkutano huo, Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo alieleza kuwa shughuli za utafiti na uchimbaji wa mafuta na gesi asilia zinaendelea katika maeneo ya kina kirefu cha bahari, mwambao wa bahari, katika maziwa na nchi kavu na kiasi cha gesi asilia kilichogundulika mpaka sasa ni futi za ujazo trilioni 43.1 hivyo inatarajiwa kuwa baada ya miaka miwili Tanzania itakuwa na gesi ya kiasi cha futi za ujazo trilioni 200.
Kuhusu sera ya gesi Waziri Muhongo alisema kuwa kwa sasa Serikali imeshaandaa rasimu ya sera ya gesi ambayo imeshajadiliwa na wadau mbalimbali wakiwemo wananchi, Taasisi za Elimu ya Juu, sekta binafsi, Bodi ya Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) na mwishoni mwa mwaka huu inatarajiwa kuwasilishwa katika Bunge la Tanzania ili ikajadiliwe na baadaye kutungiwa sheria itakayoendana na shughuli za utafutaji na uchimbaji mafuta na gesi nchini.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...