Mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba Bw. Awadh Said (kulia) akiongea na viongozi wa Jukwaa la Mamlaka na Taasisi zinazosimamia na kuthibiti ubora wa elimu nchini ulioongozwa na Mwenyekiti wake Prof. Sifuni Mchome (mwenye tai katikati). Jukwaa hilo lilikutana na Tume katika Ukumbi wa Karimjee jijini Dar es Salaam leo kuwasilisha maoni yake kuhusu Katiba Mpya.
Mjumbe wa Jukwaa la Mamlaka na Taasisi zinazosimamia na kuthibiti ubora wa elimu nchini Dkt. Primus Nkwera amabye pia ni Katibu Mtendaji wa Baraza la Elimu ya Ufundi (NACTE) akitoa maoni ya jukwaa hilo kuhusu Katiba Mpya katika mkutano na Tume ya Mabadiliko ya Katiba uliofanyika katika Ukumbi wa Karimjee jijini Dar es Salaam leo. Kulia ni Mjumbe wa Tume Bw. Humphrey Polepole na kushoto ni Mwenyekiti wa Jukwaa hilo Prof. Sifuni Mchome.
Mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba Bw. Humphrey Polepole (kulia) akiongea na viongozi wa Jukwaa la Mamlaka na Taasisi zinazosimamia na kuthibiti ubora wa elimu nchini ulioongozwa na Mwenyekiti wake Prof. Sifuni Mchome (kushoto). Jukwaa hilo lilikutana na Tume katika Ukumbi wa Karimjee jijini Dar es Salaam leo kuwasilisha maoni yake kuhusu Katiba Mpya.
Mwenyekiti wa Jukwaa la Mamlaka na Taasisi zinazosimamia na kuthibiti ubora wa elimu nchini Prof. Sifuni Mchome ambaye pia ni Katibu Mtendaji wa Tume ya Vyuo Vikuu (TCU) akitoa maoni ya jukwaa hilo kuhusu Katiba Mpya katika mkutano na Tume ya Mabadiliko ya Katiba uliofanyika katika Ukumbi wa Karimjee jijini Dar es Salaam leo. Kulia ni Wajumbe wa Tume Bw. Awadh Said (kulia) na Bw. Humphrey Polepole.
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wanataaluma wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDASA) Dkt. Francis Michael (katikati) akitoa maoni kuhusu Katiba Mpya katika mkutano na Tume ya Mabadiliko ya Katiba uliofanyika katika Ofisi za Tume jijini Dar es Salaam leo. Wengine ni Dkt. Felician Komu (kushoto) kutoka Jumuiya ya Wanataaluma wa Chuo Kikuu cha Ardhi (ARISA) na Bw. Edson Baradyana (kulia) kutoka Jumuiya ya Wanataaluma wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOMASA).
Wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba wakiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa Umoja wa Wanafunzi wa Vyuo vya Elimu ya Juu Nchini (TAHLISO) mara baada ya viongozi hao kuwasilisha maoni ya umoja huo kuhusu Katiba Mpya kwa Tume katika Ukumbi wa Karimjee jijini Dar es Salaam leo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...