Estom Sanga-Singida 

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora mhe. George Mkuchika amepongeza hatua ya Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF kubuni utaratibu mzuri wa kuwashirikisha wananchi katika ujenzi wa miradi ya maendeleo kwenye maeneo yao. 

Mhe. Mkuchika amesema utaratibu huo siyo tu kwamba unapunguza gharama bali unawafanya wananchi kuithamini miradi hiyo na kuitunza kutokana na kutumia nguvu na jasho lao katika kuitekeleza. 

Waziri huyo ameyasema hayo mwishoni mwa juma baada ya kutembelea kijiji cha Mwahango katika halmashauri ya wilaya ya Singida ambako alikagua jengo la zahanati lililojengwa na TASAF kwa kuwashirikisha wananchi kijijini hapo. 

Aidha Mhe. Mkuchika ameupongeza mkoa wa Singida kwa kusimamia zoezi la uandikishaji Walengwa wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini kwa uaminifu na hivyo kupunguza kwa kiwango kikubwa idadi ya Watu wasiostahili kujumuishwa kwenye Mpango huo kinyume cha utaratibu. 
Waziri wa nchi ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. George Mkuchika akitoka katika jengo la zahanati ya kijiji cha Mwahango katika halmashauri ya wilaya ya Singida lililojengwa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii TASAF kwa kushirikiana na wananchi wa eneo hilo. 
Mwonekano wa jengo la zahanati ya kijiji cha Mwahango katika halmashauri ya wilaya ya Singida iliyojengwa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF kwa kushirikiana na wananchi wa eneo hilo ikiwa ni mkakati wa TASAF wa kuboresha huduma za Afya kwa walengwa wake na wananchi wa eneo hilo. 
Waziri Mkuchika akipanda mche wa mti katika eneo la Zahanati ya kijiji cha Mwahango katika halmashauri ya wilaya ya Singida iliyojengwa na TASAF na wananchi . 
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. George Mkuchika (aliyesimama mbele ya kamera) akiwahutubia baadhi ya watumishi wa sekretarieti ya mkoa wa Singida wakati alipofanya ziara ya kikazi mkoani humo. 
Waziri wa nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. George Mkuchika akikagua jengo la zahanati ya kijiji cha Mwahango katika wilaya ya Singida jengo lililojengwa na TASAF ikiwa ni mkakati wa kuwasogezea huduma ya Afya wananchi na Walengwa wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini.



Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...