Chama cha wasafirishaji wanyamapori hai nje ya nchi kibiashara (TWEA) kimeiomba serikali isitishe zuio la kusafirisha nje wanyamapori hao ili wanachama wake waweze kujikwamua na hali ngumu ya maisha inayaowakabili.

Wakizungumza mbele ya Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga kwenye kikao cha Wizara na wawakilishi wa Wafanyabiashara hao waliiomba serikali isikilize kilio chao.

Kwa upande wake , Mwenyekiti wa Chama hicho, Enock Balilemwa alisema baadhi ya wanachama wakiwemo walemavu waliokuwa wamechukua mikopo benki wamefukuzwa kwenye nyumba zao baada ya kushindwa kufanya marejesho ya mikopo hiyo kufuatia zuio la biashara hiyo.

Alieleza kuwa baadhi ya wanachama wake wamejikuta kwenye hali ngumu ya kupoteza mali zao na kuingia kwenye mifarakano na wateja wao kwa vile wafanyabiashara hao walichukua pesa toka kwa wateja kama malipo ya awali hivyo wakati wa zoezi la kusimamisha biashara linafanyika liliwakuta wafanyabiashara hao wameshachukua pesa za wateja wao kama malipo ya awali.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga (kulia) akifungua kikao cha Wawakilishi wa Wafanyabiashara ya Wanyamapori hai kilichofanyika jana mjini Dodoma, ikiwa lengo la kikao hicho ni kuiomba Wizara kusitisha zuio la kusafirisha wanyamapori hai nje ya nchi kibiashara, kushoto ni Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Wanyamapori, Dkt. Nebbo Mwina
Mwenyekiti wa Chama cha wasafirishaji wanyamapori hai nje ya nchi, Enock Balilemwa akizungumza kwenye kikao cha cha Wizara ya Maliasili na Utalii na Wawakilishi wa Wafanyabiashara ya Wanyamapori hai kilichofanyika jana mjini Dodoma, ikiwa lengo la kikao hicho ni kuiomba Wizara kusitisha zuio la kusafirisha wanyamapori hai nje ya nchi kibiashara
Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Wanyamapori, Dkt. Nebbo Mwina akizungumza kabla ya kumkaribisha Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga kufungua kikao cha Wawakilishi wa Wafanyabiashara ya Wanyamapori hai kilichofanyika jana mjini Dodoma, ikiwa lengo la kikao hicho ni kuiomba Wizara kusitisha zuio la kusafirisha wanyamapori hai nje ya nchi kibiashara.
Makamu Mwenyekiti wa Chama cha wasafirishaji wanyamapori hai nje ya nchi, Fatuma Hamisi akizungumza mbele ya Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga (hayupo pichani) kwenye kikao cha cha Wizara ya Maliasili na Utalii na Wawakilishi wa Wafanyabiashara ya Wanyamapori hai kilichofanyika jana mjini Dodoma ikiwa lengo la kikao hicho ni kuiomba Wizara kusitisha zuio la kusafirisha wanyamapori hai nje ya nchi kibiashara.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...