Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Mama Samia Suluhu Hassan akipata maelezo kutoka kwa kikundi cha Walemavu kutoka Mwembe Makumbi kinachojishughulisha na kutengeneza viatu wakati alipotembelea maonyesho ya walemavu katika uwanja wa Skuli ya Uzini.

Leo ni Siku ya Kimataifa ya Watu wenye Ulemavu Duniani na ambapo Kitaifa siku hii inaadhimishwa Mkoa wa Kusini Unguja na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano ni mgeni rasmi.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Mama Samia Suluhu Hassan akifafanua jambo kwa kikundi cha Walemavu kutoka Mwembe Makumbi kinachojishughulisha na kutengeneza viatu wakati alipotembelea maonyesho ya walemavu katika uwanja wa Skuli ya Uzini.

Leo ni Siku ya Kimataifa ya Watu wenye Ulemavu Duniani na ambapo Kitaifa siku hii inaadhimishwa Mkoa wa Kusini Unguja na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano ni mgeni rasmi.
Sehemu ya Maandamano ya Walemavu yaliofanyika Uzini, wilaya ya Kati, mkoa wa Kusini Unguja wakati wa maadhimisho ya siku ya walemavu duniani. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
 Sehemu ya Watu wenye ulemavu wakimsikiliza kwa makini Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania alipokuwa akihutubia kwenye kilele cha siku ya kimataifa ya maadhimisho ya watu wenye ulemavu yaliofanyika kwenye viwanja vya skuli ya Uzini, wilaya ya Kati mkoa wa Kusini Unguja, Zanzibar. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akikabidhi kiti maalum cha kutembelea walemavu (Wheel Chair) kwa   Bi. Hidaya Shaib Muombwa ambacho kilipokelewa na ndugu yake kwa niaba wakati wa kilele cha maadhimisho ya siku ya walemavu duniani katika viwanja vya Skuli ya Uzini, mkoa wa Kusini Unguja.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimkabidhi mafuta maalum ya ngozi Bw. Hussein Ussi Ali wakati wa kilele cha maadhimisho ya siku ya walemavu duniani katika viwanja vya Skuli ya Uzini, mkoa wa Kusini Unguja.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...