adaktari Bingwa wa magonjwa ya Moyo kwa watoto kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI)na wenzao wa Taasisi ya Open Heart International (OHI) ya nchini Australia wakifanya upasuaji kwa mtoto ambaye vyumba vyake vya moyo havijakamilika na hivyo damu kwenda kwa wingi kwenye mapafu katika kambi ya siku tano ya matibabu ya moyo iliyomalizika leo katika Taasisi hiyo.Picha na JKCI
Madaktari Bingwa wa Upasuaji wa Moyo na mishipa ya damu kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakimfanyia mgonjwa upasuaji wa kupandikiza mishipa ya damu kwenye moyo (CABG – Coronary Artery Bypass Grafting) katika kambi maalum ya siku tano ya matibabu ya moyo iliyomalizika leo katika Taasisi hiyo. Jumla ya wagonjwa 16 wamefanyiwa upasuaji na hali zao zinaendelea vizuri kati ya hao watoto ni tisa na watu wazima saba.
Mwanzilishi wa Taasisi ya Open Heart International ya nchini Australia Russel Lee akiongea na waandishi wa Habari kuhusu upasuaji wa moyo wa mtoto ambao umekaa upande wa kulia na mishipa yake ya damu chafu na safi imeingiliana katika upasuaji huo wameweza kulinda mapafu yalikuwa yanapokea damu kwa wingi kutoka kwenye mishipa ya moyo na mtoto kawekewa kifaa ambacho kitamsaidia moyo wake kufanya kazi vizuri (Pace Maker). Kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi na kushoto ni Daktari Bingwa wa Upasuaji wa Moyo kwa watoto Godwin Sharau.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...