Na Chalila Kibuda , Globu ya Jamii

TAFITI  za kisayansi zikitumika kwa ufasaha  zitasaidia kupunguza magonjwa kwa binadamu kwa asilimia 40. Tafiti hizo ni pamoja na wananchi kupata taarifa za masuala ya afya pamoja na kufuata ushauri wa wataalam juu ya kujiepusha na magonjwa mbalimbali.

Hayo yamebainishwa leo jijini Dar es Salaam na  Rais wa Tanzania Health Summit, Dk. Omary Chillo wakati akitoa taarifa kwa waandishi wa habari juu ya Mkutano wa  Kitaifa  wa Sekta ya Afya nchini utakaofanyika Novema 14 hadi 15 mwaka huu katika Ukumbi wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam.

Chillo amesema kuwa mkutano huo utajadili changamoto za sekta za afya  nchini pamoja na kuboresha sekta hiyo ili iweze kuhudumia jamii kwa upatikanaji wa huduma bora za afya. Amesema mkutano huo utatoa mapendekezo yanayoonesha suluhisho la mjadala watakayojadili na litaandikwa kwenye kitabu na kusambazwa kwa taasisi za afya na kufuatilia utekelezaji wake.
Katibu wa Tanzania Health Summit, Rebecca John akizungumza juu ya usajili wa ushiriki wa mkutano wa sekta ya afya utakaofanyika Novema 14 hadi 15 mwaka huu katika Ukumbi wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere(JNICC) jijini Dar es Salaam. wengine ni Rais wa Tanzania Healt Summit, Dk. Omary Chillo pamoja na Mwakilishi wa APHFTA, Joseph Mhagama.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...