WAKAZI wa Manispaa ya Dodoma wameshauriwa kuhudhuria Mkutano wa
Baraza la Madiwani ili kupata taarifa za miradi mbalimbali ya maendeleo
inayotekelezwa na Manispaa yao na kujua kazi inayofanywa na Madiwani
waliowachagua.
Wito huo umetolewa na Naibu Meya wa Manispaa ya Dodoma Jumanne
Ngede kuelekea Mkutano wa Baraza hilo wa kisheria kwa robo ya kwanza
ya mwaka wa fedha 2017/18 utakaopokea taarifa mbalimbali za Manispaa
hiyo kitakachonyika Oktoba 31 mwaka huu katika ukumbi wa Manispaa.
Naibu Meya Ngede alitoa wito huo wakati alipoongoza Mkutano wa awali
wa Baraza la Madiwani la Manispaa hiyo lililopokea taarifa za utekelezaji
wa miradi kutoka katika Kata zote 41 za Manispaa ya Dodoma Oktoba 25
mwaka huu.
Aliiagiza Ofisi ya Mkurugenzi wa Manispaa ya Dodoma kuongeza
matangazo kwa wananchi kuhusu tarehe ya Mkutano huo ili waweze
kuhudhuria kutokana na umuhimu wa mkutano huo ambao ni wa wazi.
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Dodoma Godwin Kunambi (kushoto) akizungumza wakati wa Mkutano wa awali wa Baraza la Madiwani wa Halmashauri hiyo Oktoba 25 mwaka huu. Katika ni Naibu Meya wa Manispaa hiyo Jumanne Ngede na kulia ni Afisa wa Serikali za Mitaa Kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Emmanuel Kuboja.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...