Naomba kuwasilisha mtazamo wangu juu ya suala la Usalama wa Raia kwa watu wa Kigamboni
Kufutatia kitendo cha wanafunzi wa IFM kuandamana na kusimamisha shughul;i za kivuko kwa muda, tatizo hili sasa limepata sura mpya, na limepata kufika kwenye masikio ya watu ambao wamepewa dhamana ya kulinda raia na mali zao.
Wimbi la uhalifu kigamboni limekuwa kubwa sana na haswa suala la hawa vijana wanaoshinda Beach (Beach Boys) kufanya mambo ambayo kimsingi yangeweza kuzuiliwa na polisi wetu. Tatizo ni "business as usual attitude" kwa askari wetu.
Tumeshuhudia watalii wakiibiwa vitu vyao na kujeruhiwa vibaya na vijana hawa, tumeshuhudia vijana hawa wakipora mabegi ya wanafunzi, wakiwa na malengo ya kuibia wanafunzi hawa laptop zao. Askari wanafahamau vyema kabisa mambio haya. Ni askari gani wa kigamboni asiyejua kijiwe cha minazi mikinda?
Bhangi, unga na aina zzote za dawa za kulevya zinuzwa na kutumiwa hapo. Ni askari hawa hawa wanawahi kwenda huko pindi ukitokea uporaji wa vitu hivyo (nimepata kusikia wanawahi mgao!!!????). Sasa leo tunasikia wanafunzi wanavamiwa wakiwa vyumbani mwao, wanaporwa na kudhalilishwa.
Ni nani asiyejua kuwa ili kuondoa wimbi hili ni lazima kuboresha doria kwenye fukwe hizi za kigamboni? Ni aibu kwa nchi kwa ujumla kufuga kundi kubwa la vijana wala unga nje tu ya uwanja wa Ikulu, pale karibu na soko la samaki? Nje ya ikulu vijana wanavuta unga. Je usalama wa kilometre 1000 kutoka ikulu ilipo ukoje?
Maandamano ya wanafunzi Kigamboni yafungue macho ya wahusika kuhusu hali halisi ya usalama kigamboni. Wananchi wa kibada wamepitia kipindi kigumu kiasi kwamba karibu kila mwanannchi aliishia kumiliki silaha, na sio moja kwani hali ilikuwa mbaya kupita kiasi. Walinzi wa Bar wanauwawa, madereva wa taxi wanauwawa.
Nyumba zinavamiwa kila leo. nk. Tunaona polisi wakipita kufanya doria usiku, lakini basically doria hii hulenga bar ambazo hazijafungwa baada ya saa tano (saa sita weekends). Kweli nguvu hii ya kukamata wahudumu wa bar ikielekezwa kusaka wahalifu hatutapata nafuu ya kiusalama? Nadhani bado tuna nafasi kubwa sana ya kuboresha usalama kabla hali haijawa mbaya.
Kila wakati polisi wanawakumbusha wananchi kuwa wasichukue sheria mkononi. Tunategemea nini kama wananch wanamawazo kuwa Polisi wanashirikiana na wezi?Unawezajae kuelewa unapoambiwa kuwa wezi walitumia zaidi ya saa mbili ndani ya hostel ya wanafunzi huku wanafunzi wakike wakipiga kelele kuomba msaada?
Ndugu zetu polisi, kodi zetu zinapaswa kutulinda, na si kushiriki katika vitendo viovu pamoja na waovu. Wezi wote wa ferry, na haswa hawa beach boys wanajulikana. Shukeni kule chini, fanyeni doria, tumieni mbinu zenu za kiupelelezi mlizofunzwa kwa kodi zetu kuwafichua na kuwafikisha waovu hawa sehemu inayostahili na sio huku mitaani. Huku sisi tunahitaji amani, na tunahitaji kufanya mipango ya maendeleo, na sio kulala na hofu kila siku.
Naomba mamlaka zitekeleze wajibu wao wa kikatiba, kulinda maisha ya raia na mali zao. Sio kulinda tu maisha ya watawala kwa misafara mirefu isiyo na sababu wala tija kwa taifa letu.
Naomba kuwasilisha
sio huku tu ndugu yangu..tenda tandale na mwananyamala issue ni hizo hizo..
ReplyDeletejeshi la polisi Tanzania ni la hovyo tu,sijui kwa nn tanzania yetu watu hawataki kuwajibika, mbona enzi za mwalimu watu walikua serious sana na kazi zao???
polisi wengine wanasaidia hata kusafirisha baadhi ya magunia ya bangi kwenye magari yao, wakijadai eti wameyakamata,
jamani inauma sana...
Ndugu mdau asante kwa nakala yangu muhimu kwa jamii na tumuombe mungu atusaidie lakini kwa serikali yetu nahisi nivipofu na viziwi sbb kuna maswala mengi ya usalama jeshi la polisi halifanyi kazi kabisa!Kama hawakuona pale kivukoni basi nivipofu lakini na sisi siwajinga tunajuwa kama wanashirikiana na wahalifu!Ukiangalia pia kwenye kung'olewa mpaka vitu kwenye magari kuna sbb kutowa spareparts zilizotuka kama polisi wanashindwa kufanya kazi yao!majambazi unashangaa vipi wanashindwa kukamatwa wakati ukiangalia kuna uzembe mwingi unafanywa na polisi sbb ya kugawana mali inayoporwa!halafu pia ninashangaa bunge imesaidia sana mambo mengine lakini kwenye usalama hakuna hakuna anayepiga makelele!Polisi jamani tanzania ni uoza!!nilisema muda kwamba said mwema awajibike lakini viongozi wake wajuu pia hawafai!!swala la usalama kigamboni nimeshaona hapa zaid ya mara 10 vipi usalama wanadharau raia walipa kodi?
ReplyDeleteAhsante sana mdau kwa kutoa taswira halisi ya maisha ya kigamboni. Wengine sisi ni residents watarajiwa kwani tayari tumeshanunua viwanja na tunajitayarisha kujenga.
ReplyDeletePolisi munaochukua mgao huo wa wizi na udhalilishaji mujue muna dhambi kubwa sana, lakini hayo hayataishia kwenye dhambi tu. Kamanda Kova tunataka hatua zichukuliwe kama walivyosema wanafunzi hao.
Mimi nilikuwa nikidhani wanafunzi hao ni wakorofi tu lakini kutokana na maelezo ya mdau walikuwa na haki kabisa ya kufanya hayo maandamano ili kujisalimisha wao na maisha ya raia wengine.
WAHALIFU WAKUBWA NI HAWA DONYO, MBOKOO, NA POLISI KIGAMBONI WANAWAJUA VIZURI WAMESHAFANYA UHALIFU KARIBU NUSU YA KIGAMBONI KWA WANAFUNZI KWANINI WASHINDWE KUWAKAMATA? MHESHIMIWA KOVA KIGAMBONI YOTE HAIKO SALAMA WANAFUNZI NA RAIA WAMEPIGWA MAPANGA NA WANAUGULIA NDANI NA TAARIFA POLISI ZIPO. ENEO LA MIDIZINI NDIO SEHEMU KUBWA AMBAYO TUMEKUMBWA NA WIZI HUU KISA NI HILI POLI LA JESHI AMBALO LA MIZINGA NDIO SEHEMU WANAYOJIFICHA TOKA MINAZI MIKINDA HADI JESHINI WANAPITA BILA KUKAMATWA HATA NA JESHI, WEZI NANAIBA NA WANAPITA JESHINI WANATOKE MIKADI BEACH BILA HATA WOGA NA NDIO SEHEMU WANAYOJIFICHA, TUNAOMBA JESHI LA MIZINGA LIFANYE ULINZI ENEO LAKE LA KAMA WAMESHINDWA KULINDA WAPISHE RAIA WAJENGE ILI TUPATE URAHISI WAKUWAKAMATA HAWA WEZI.
ReplyDeleteTULIYEATHIRIKA.
Mie ni mfuata sheria na niko mbali na siasa. Ila nasema: HAKI YA MUNGU iwapo mtoto wangu wa kike au wa kiume anadhalilishwa na kuwa raped mwenyewe ningeenda hapo kuwawinda hao jamaa na yeyote atakayefanana nao atarudisha roho yake Pia wafikapo Polisi lazima niongoke na kati zao. Na risasi moja najimalizia mwenyewe. Mkuu wa Polisi afukuzwe kazi ili liwe funzo kwa wengine: huwezi fanya kazi, ondoka. Blackmpingo
ReplyDeleteNdugu yetu Mhe. Raisi Jakaya Kikwete,
ReplyDeleteUmezidi kuwa na huruma na kuwafanyia Uungwana na Uislamu sana hao jamaa MATEJA WASIO BEBEKA KAMWE ambao ni Wahalifu wenyewe hapo nje ya Ukuta wa Makazi yako!
Hao jamaa wanashinda kutwa wakigalagala mchangani ufukweni na Misokoto ya mabangi huku wakijidunga sindano za madawa ya kulevya na kufanya Ulawiti na Ubakaji na wizi!
Kiongozi wetu katika Ikulu zote Duniani wenzako kuchukua zaidi ya Kilometa 3 kama mwisho wa mchezo mchezo kwa wapitaji njia holela kama hao Mateja hapo Beach!
KIUTARATIBU KWA MAKAZI YAN KAWAIDA META 1,000 AU KILOMETA MOJA NDIO JIRANI ZAKO, HIVYO HATUTEGEMEI KIONGOZI WETU UBEBESHWE MAJIRANI WA AJABU KAMA HAO JAMAA AMBAO NDIO IMEKUWA CHANZO CHA SHIDA HII.
NA KWA KUWA UUNGWANA UMEKUZIDI KIONGOZI WETU INAKUWA VIGUMU KUFANYA MAAMUZI MAGUMU DHIDI YAO KAMA WANAVYO FANYA VIONGOZI WENGINE WENZAKO DUNIANI.
TUNAOMBA MAAFISA HUSIKA MUONDOE UOZO HUU WA HAWA WATU NA NYENDO ZAO CHAFU KARIBU NA MAKAZI YA RAISI WETU!!!
Naunga mkono unachoongea, nimeandika maoni kwenye picha zile Polisi wanapiga wanafunzi walipokuwa wanaandamana, kwamba nimechukizwa mno na serikali kwa kitendo hicho mpka nimeamua kuingilia siasa. Utawapigaje watu namna hiyo bila kosa? wakati huo huo majambazi wanatesa tu?. Kichwa changu kibovu siwaelewi Wabongo yaani tunaona ni sawa tu kwa watu kupigwa?, ambapo angekuwa hata mbwa anapigwa namna hiyo nina uhakika watu wangeingilia kati. Yaani vitendo vya maaskari kupiga watu vinatuamithisha wengine kwa moyo mkubwa sasa. Yaani yule jamaa anyepiga wanafunzi mateke lazima apelekwe kortini kwa kuika haki za binadamu. Ni aibu kwa Taifa kutesa raia wake namna hii. Viongozi wako wapi, hawaoni hata aibu?
ReplyDeleteWatanzania tunataka kuungana na wanafunzi maandamano tena Dar nzima mnasemaje?
ReplyDeleteMM NAONA KWANZA WAPATEKANE HAO WAHALIFU ALAFU KUU WA KITUO AFUKUZWE KAZI KAMA ALIWEZA KUPUUZA MALALAMIKO YA WANAINCHI INAMAANA AFAI KWA LOLOTE.WANAZARAU WANANCHI KWA KUWA WAO WANAISHI KWENYE KOTA TUNAZOJENGA KWA KODI ZETU,ANGEKUWA POLICE NDIO AMEBAKWA AU AMEUWAWA HAPO KIGAMBONI PASINGE KALIKA ILA KISA NI WANAFUNZI NA RAIA WANYONGE YANI HAPO HATA HUYO KOVA ANGEKUWA ULAYA HANA KAZ.AWEZI FANYA UCHUNGUZI MPAKA MAANDAMANO.
ReplyDelete
ReplyDeleteafu cha kushangaza, hawa viongozi wetu na mpaka huyo kamanda mkuu wa uwajibikaji nae analindwa. Ila likija swala la wanachi wao. Hapo hawaoni wajibu wao. Na wanasahau kwamba wapo katika hiyo kazi kwa maslahi ya wanchi. Na mishahara wanayolipwa ni kodi za wanachi wao. Alafu wanaendekeza uzembe wa watu wajinga. Kama hawa wezi.vibaka.mjambazi. hawa ni watu hatari sana katika jamii yoyote.
Mimi naamini mapolisi wengi ni waovu.nawahisi kama organised crimininals.hakuna maandamano ya amani yanayokataliwa au kwa raiaa wema kuunda vikundi vya kujilinda ila inatakikana watu wajipange kikamilifu.kwanini haturudishi sungusungu?!chadema ungana nawananchi kuunda maandamano kwani ccm wanahisi bado ni chama pekee kitafanya kinavotaka.
ReplyDeletejamani nawaomba wabunge waingilie kati hili swala watuwakilishe bungeni kuhusu uonevu wa raia kwani raia ukiandamana kudai haki yako unaishia kupigwa au kuuliwa bila hatia na polisi ,ZITO KABWE NAKUAMINIA SANA HUKO WAPI PLEASE NENDA KATUSAIDIE KUTUSEMEA HILI SWALA LA UONEVU WA RAIA unaofanywa na polis naona wananchi tutasikilizwa pili,nilishuhudia mwanafunzi anaibiwa live baada ya kuvuka kwenye pantoni anapiga kelele no body care polisi pia hawajali nilikuwa mbali kidogo nakaribia washakimbia na kumwibia mwanachuo tena wa ifm namsaidia mwanafunzi kwenda kulipoti yaani unaweza kutukana polisi hawajali kabisa ni matukio ambayo wameyazoea na wanawajua hao wezi na siajabu wanagawana nao hivyo vitu wanavyoiba inasikitisha sana jamani.tunajiita nchi ya amani amani iko wapi!!!!
ReplyDeleteTATIZO KUBWA NI POLISI KUKOSA UADILIFU NA HOFU YA MUNGU. WAMEKUWA WASIO NA ELIMU AMA WELEDI WA KAZI NA WAJIBU WAO/WAZEMBE/ WENYE TAMAA ZA UTAJIRI WA HARAKA/WAONGO/KANDAMIZI HASA KWA WENYE HAKI/WAKISHIRIKI UOVU NA WAKORA WAKATI WOTE.... WATATOA VISINGIZIO VYA GARI/MAFUTA NA AMA WAKO MBALI KUMBE WANAACHIA TUKIO LITOKEE KISHA WANAFUATA MGAO WAO!! LAANA NA AIBU YAO NA VIZAZI VYAO MILELE.
ReplyDeletevery stupid comments, no solutions wewe unaetega kazi na kuangalia michuzi mchana na kufungulia nyimbo ofisini umeshaiibia serikali, kodi unayolipa ni ya kununulia dawa na kujengea madarasa sio ya kukulinda wewe.
ReplyDeletekwa kweli jeshi letu la tanzania limekuwa ni aibu,hivi kama polisi wamefikia hatua ya kushirikiana na vibaka, wanainchi wanapaswa kukimbilia wapi? mimi naona jeshi hili linahitaji kusukwa upya, kwani nidhamu ya jeshi hili haipo tena.
ReplyDeletevitendo hivi vimekithiri kigamboni na Polisi kigamboni hawafanyi chochote, watu wengi imebidi wahame nyumba zao walizojenga wenyewe kigamboni na kwenda kupanga maeneo mengine nje ya kigamboni,hii ni kwamba Polisi wenyewe wanahusika, na wanawajua vizuri wahalifu wote... ndo maana hapa katikati watu waliamua wakiwakuta wanawaua tu.. maana hata ukiwapeleka polisi hakuna kinachofanyika.... kuna watu walikamatwa usiku wapo kwenye shughuli zao za wizi, walikuwa na gari kbs,kulifuatilia hilo gari ni la polisi fulani ambaye ana cheo tu, sasa hapo unategemea hao wahalifu wataisha?
ReplyDeletena hao wahalifu ni group ya watu, wameajiriwa kbs, wanatoka kwenda kazini kama wengine, kumbe wanaenda kusuka mipango,waingie wapi na wafanye nini... Polisi wanajua kila.
Yote hii Polisi ni njaa kuwaivalia njuga na kukosa akili nzuri.
ReplyDeleteHivi asasi za kutetea haki za binadamu ziko wapi katika maswala haya.Mbona wanashindwa kutoa tamko la kulaani vitendo hivi. Wao wanashabikia kutetea wanasiasa tu.
ReplyDelete