Faida ya Hifadhi endelevu ya Mazingira. Pichani ni eneo la Ngaresero Wilaya ya Meru ambapo kuna uhifadhi mzuri wa mazingira. Hata hivyo eneo hilo limeanza kuvamiwa na wananchi kwa shughuli za kibinadamu na kuhatarisha uhai wake. Waziri Makamba ametembelea eneo hilo na kumtaka Bw. Timoth Leach mmiliki wa Ngaresero Mountain Lodge kufanya ukaguzi wa mazingira mara moja ili kubaina matumizi sahihi ya rasilimali maji.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mh. January Makamba akipanda mti wa kumbukumbu nyumbani kwa Hayati Edward Moringe Sokoine. Waziri Makamba yuko katika ziara ya kikazi Mkoani Arusha na alitembelea msitu wa Enguiki na Lendikinya kisha alizungumza na wananchi katika mkutano wa hadhara.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...