Kitengo kinachoshughulika na ukuaji wa benki za ki-Islam The Islamic Corporation for the Development of the Private Sector (ICD) kina mpango wa kufungua benki mpya ktk nchi za Mali na Benin mwaka huu 2013.
Mkurugenzi mkuu wa ICD Mh. Khaled Mohammed Al- Abood akizungumza ktk mkutano unaohusiana na benki hizo uliofanyika nchini Djibouti, alinukuliwa akisema kwamba ICD itausaudia uchumi huo ktk maeneo ambayo bado huduma zake ni ndogo.
Katika kulifafanua hilo alisisitiza kwamba shirika hilo lina mpango wa kutoa million 200 Sukuk (Islamic bonds) kwa serikali ya Senegal kwa ajili ya kuiwezesha nchi hiyo kutoa huduma ya benki zinazofuta sheria ya kiislam.
Alinukuliwa akisema ‘zaidi ya asilimia 50 ya wakazi wa Africa ni waislam na mahitajio ya huduma hiyo ni makubwa sana lakin kuna changamoto nyingi zinazohusiana na kufika kwa huduma hiyo ktk maeneo husika. Tabia ya benki zinazofuata sheria za ki-Islam zinaiweka ktk nafasi nzuri ya kua mbadala wa benki zisizofuata sheria za ki- Islam na ambazo zimekuwepo kwa muda mrefu.
ICD ilikua na matumaini makubwa ya kufanya miradi mingi Africa kwa kua inafahamu kwamba Africa inahitaji sana miundombinu. ‘Kitu ambacho nchi za Afrika inakihitajia sana kwa ajili ya maendeleo ni miundombinu, barabara, nyumba, mashule na hospitali’ alisema ndugu Al-Abood.
Karinbu nchi kumi barani Africa zimeshakubaliwa kupata msaada wa ICD kati ya mwaka 2010-2012 na kuna zile ambazo zimefaidika sana kama vile Mauritania, Sudan, Gabon, Gambia na Mali.
Kwa maelezo zaidi kuhusu benki zinazofuata sheria za ki-Islam tembelea http://ijuebankyakiislam.blogspot.com
Hiyo Kauli kwamba,zaidi ya asilimia 50% ya Waafrika ni Waislamu,hiyo Sensa ilifanyikia wapi na mwaka gani,na nani aliye ifanya? tuache ushabiki kwenye masuala ya kiuchumi jamani! Mabenki hayo ya Kiislamu ni muhimu pia katika maendeleo ya watu!Hakuna anayebeza kuhusu hilo.Tusipende kutia chumvi,hata pasipo husika!kuna mwingine anaweza kuibuka akasema,hata kama ni kweli wao ndio wengi,"So What?".
ReplyDelete