Katibu Mkuu wa Bodi ya Wadhamini ya Tanzania Motorcycles Movement Association (TAMOSA), Kizito Msangya pamoja na Mh. Devotha Minja (MB) wakimsikiliza kwa makini mtaalam kutoka Jeshi la Polisi (Usalama Barabarani) (hayupo pichani) wakati akielezea umuhimu wa Bodaboda kufuata sheria kuhakikisha usalama wao barabarani. Katibu Mkuu wa Tamosa alisema lengo kuu la semina hii ilikuwa kuwakutanisha wadau mbalimbali katika sekta ya usafirishaji ili kuibua fursa mbalimbali zinazoweza kupatikana, lakini pia kuhakikisha Bodaboda ni usafiri salama, wa haraka unaopendwa na kutumika kwa maendeleo ya wananchi na taifa kwa ujumla aliongeza pia kauli mbiu ya Tamosa ni "Bodaboda ni Huduma Ajira na Uchumi" Aidha alieleza wadau waliolikwa kwaajili ya kuwasilisha mada ni Jeshi la Polisi, TRA, SUMATRA, Mabeki ya Biashara pamoja na Mifuko ya Pensheni
Baadhi ya wajumbe wa Bodi ya Tamosa Bw Aloyce Ntukamazina na Mh Joyce Mukya (MB) wakishiriki katika semina hii maalum kwa sekta ya usafirishaji ambayo imetoa ajira kwa vijana takriban 4,000,000 nchi nzima.
Baadhi ya wadau mbalimbali waliolikwa katika semina hii maalum wakifuatilia kwa makini mada zilizokuwa zikiwasilishwa na wahusika.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...