Mtaalamu wa Afya na Mazoezi ya viungo kutoka Chama Cha Wafanya Mazoezi Tanzania Waziri Ndonde akiwaelekeza wananchi waliokuwa wanasubiri kwenda kupima magonjwa ya moyo katika banda la Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) umuhimu wa kufanya mazoezi na aina ya mazoezi wanayotakiwa kuyafanya. Wizara ya Afya, Jinsia, Wazee na Watoto hivi karibuni ilizindua kampeni ya kitaifa ya kufanya mazoezi na kupima afya bila malipo kwa muda wa siku mbili kwa wananchi wa mkoa wa Dodoma.
Mtaalamu wa Dawa na Tiba kutoka Hospitali ya SANITAS Dk. Sajjad Fazel akiwafundisha wananchi waliokuwa wanasubiri kwenda kupima magonjwa ya moyo katika banda la Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) aina ya vyakula bora wanavyotakiwa kula ili waepukane na magonjwa yasiyoambukiza. Wizara ya Afya, Jinsia, Wazee na Watoto hivi karibuni ilizindua kampeni ya kitaifa ya kufanya mazoezi na kupima afya bila malipo kwa muda wa siku mbili kwa wananchi wa mkoa wa Dodoma.
Afisa Muuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Andrew Kabeho akimpima mapigo ya moyo Afisa Muuguzi wa Hospitali ya mkoa wa Dodoma Mariam aliyefika katika banda la Taasisi hiyo kwa ajili ya kupima magonjwa ya moyo. JKCI ilishiriki katika kampeni ya kitaifa ya kufanya mazoezi na kupima afya bila malipo iliyoandaliwa na Wizara ya Afya, Jinsia, Wazee na Watoto na kufanyika katika uwanja wa Jamhuri jumla ya wagonjwa 408 walihudumiwa katika banda hilo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...