Kamishna Mteule wa Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Dawa za kulevya,Rogers William akizungumza wakati wa uzinduzi rasmi wa mazoezi kwa wananchi mkoa wa Kilimanjaro,uzinduzi uliofanyika katika uwanja wa Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi.

Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii Kanda ya Kaskazini.


SIKU chache  baada ya kuteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt John Pombe Magufuli kuwa Kamishna wa mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya (Drug Control and enforcement Authority), Rogers William ameanza kutema cheche dhidi ya Wafanyabiara na watumiaji wa dawa za Kulevya.

Kamishna huyo  ametangaza kushughulika kikamilifu na baadhi ya wafanyabiashara mkoani Kilimanjaro,wanaowatumia wanawake wajasiriamali wanaosafirisha mazao kwenda mikoani, kubeba Mirungi ama Bangi ndani ya mizigo ya mazao.
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro,Saidi Meck Sadiki akizungumza juu ya Dawa za kulevya mara baada ya kumalizika uzinduzi rasmi wa siku ya mazoezi ikiwa ni utekelezaji wa agizo la Makamu wa Rais ,Samia Suluhu Hassan.

William alitoa kauli hiyo wakati wa mazoezi katika uwanja wa Chuo kikuu cha Ushirika Moshi (MoCU) baada ya mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro , Saidi Mecky Sadiki kutoa nafasi kwa Mkuu huyo wa usalama wa taifa mkoa wa Kilimanjaro , baada ya kumpongeza kwa kuteuliwa kwake.


“Tunayo orodha ya wafanyabiashara wasio waaminifu na wengine wananchi wa kawaida wanaowatumia wanawake wasio na hatia kusafirisha dawa za kulevya kama Mirungi na Bangi kwenda mikoani….hilo nitahangaika nalo mara nitakaporejea mkoani hapa katika mapambano dhidi ya vita hii”alisema Sadiki.

Kauli ya William ilifuatia baada ya Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro,Saidi Meck Sadiki kulitaka jeshi la Polisi kufaya uchungizi wa kina ili kuwaachia baadhi ya wanawake watakaobainika kutokuwa na hatia ama kufahamu kama walitumika kusafirisha dawa za kulevya bila ridhaa yao.
Kamanda wa Polisi mkoa wa Kilimanjaro,Kamishna msaidizi Mwandamizi wa  Polisi,Wilbroad Mutafungwa akitoa salamu za jeshi hilo katika uzinduzi huo.


Akizungumzia kuhusu Dawa za kulevya,Sadiki alisema vita dhidi ya dawa  za kulevya za aina mbalimbali kwa mkoa wa Kilimanjaro imeanza muda mrefu na tayari zaidi ya watuhumiwa 689 wa dawa hizo wanashikiliwa katika kipindi cha mwaka mmoja kuanzia Januari mwaka 2016 hadi Januari 2017.

Sadiki alisema vita hiyo ni ya kudumu yenye changamoto kubwa baada ya mkoa wa Kilimanjaro kuwa na njia nyingi za Panya katika mipaka baina ya Tanzania na Kenya, huku ikizingatiwa kwamba Kenya inalitumia zao la Mirungi kama biashara halali.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...