Na Daudi Manongi-MAELEZO.
Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii Meja.Gen Gaudence Milanzi amewaasa wafugaji kuacha kuingiza mifugo katika hifadhi za taifa ili kuzitunza hifadhi hizo.
Katibu Mkuu uyo aitoa wito huo wakati akizungumza baada ya kufanya matembezi ya kupinga ujangili unaofanywa dhidi ya Tembo  ya kilometa 5 kutoka Ubalozi wa China mpaka Hoteli ya Sea Cliff  ambapo wageni mashughuli kama Rais Mstaafu wa awamu ya tatu Mhe.Benjamini William Mkapa alishiriki.
“Hifadhi za taifa hapa nchini hazina budi kulindwa na kutunzwa ili vizazi vijavyo viweze kuzifaidi kwani maeneo hayo yametengwa kwa ajili ya wanyama pori pekee na siyo kwa mifugo na hivyo kila mwananchi analo jukumu la kuyalinda mazingira haya,”Aliongeza Mej.Gen Milanzi.

Awali akizungumza katibu mkuu huyo alisema kuwa Serikali ina mkakati mkubwa wa kuhakikisha inashirikiana na nchi zingine katika kutokomeza kabisa Ujangili wa pembe za ndovu nchini.
Aidha aliishukuru Serikali ya Jamhuri ya watu wa China kwa kuwa mstari wa mbele katika kupambana na ujangili wa pembe za ndovu ikiwemo upigaji  marufuku biashara ya pembe za ndovu na viwanda vya kuchonga pembe hizo ifikapo mwezi machi Mwaka huu.
 Rais Msataafu wa Awamu ya Tatu wa Tanzania, Benjamin William Mkapa akizungumza mara baada ya kupokea Matembezi kwa ajili ya kupinga ujangili ya Walk for Elephant Dar es Salaam 2017 leo jijini Dar es Salaam. Matembezi hayo ya kilomita tano yameratibiwa na Asasi ya Tanzania – China Promotion Association (TCFPA) na Ubolozi wa China ambapo yalianzia Ofisi za Ubalozi wa China na kuishia katika Hotel ya Sea Cliff.
 Balozi wa China nchini Dkt. Lu Youqing, akizungumza kabla ya kuanza matembezi  ya Walk for Elephant Dar es Salaam 2017 leo jijini Dar es Salaam. Matembezi hayo ya kilomita tano yana lengo la kuhamasisha upingaji wa ujangili na mauaji ya Tembo.
 Katibu Mkuu wa Asasi ya Tanzania – China Promotion Association (TCFPA) akitoa maelekezo kuhusu matembezi ya  Walk for Elephant Dar es Salaam 2017 leo jijini Dar es Salaam. Matembezi hayo ya kilomita tano yameratibiwa na asasi hiyo kwa kushirikiana na Ubolozi wa China ambapo yalianzia Ofisi za Ubalozi wa China na kuishia katika Hotel ya Sea Cliff.
 Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Ally Hapi (kushoto) akisalimiana na Balozi wa China hapa nchini Dkt. Lu Youqing wakati wa matembezi ya Walk for Elephant Dar es Salaam 2017 yaliyofanyika leo jijini Dar es Salaam. Lengo la matembezi hayo ni kuhamasisha jamii kupinga ujangili na mauaji ya Tembo.
 Balozi wa China nchini Dkt. Lu Youqing, akiwaongoza mamia ya wakazi wa jiji la Dar es Salaam kufanya mazoezi kabla ya kuanza matembezi  ya Walk for Elephant Dar es Salaam 2017 leo jijini Dar es Salaam. Matembezi hayo ya kilomita tano yana lengo la kuhamasisha upingaji wa ujangili na mauaji ya Tembo. Kwa habari kamili BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...