Wajasiriamali wadogo na wakati(SME) nchini wametakiwa kuboresha huduma zao ikiwa pamoja na kuzalisha bidhaa zinazoweza kushindana katika soko la ndani na nje ya nchini. 
Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Bw.Charles Mwijage amesema dawa pekee kwa wajasiriamlai kushinda masoko ni kutengeneza bidhaa zenye ubora wa hali ya juu. 
“Nchi yeyote duniani ambayo imepiga hatua ya viwanda na maendeleo , mchango mkubwa umetoka kwa wajasiriamali,” alisema Bw.Mwijage

Akifungua duka la Mikono fair trade Shop linalomilikiwa na Mikono Cultural Heritage Ltd ambalo linauza bidhaa zinazotengenezwa na wajasiriamali wadogo wa hapa nchini, Waziri Mwijage alielezwa kulidhishwa na bidhaa zilizokuwa dukani hapo. 
Alisema Serikali itatoa ushirikiano kwa wajasiriamali katika kuwakuza kwa kuwatafutia masoko ya bidhaa zao na pia kuwapatia elimu zaidi ya namna ya kuboresha bidhaa ili kuwendana ushidano wa soko.

“kazi kubwa iliyopo ni kuhakikisha bidhaa hasa za kitamaduni nchini zinapatikana katika duka hili,” alisema Waziri Mwijage na kuongezea kuwa hivyo ndivyo yanavyofanya maduka trade fair duniani kote.

Alisema kampuni hii inashirikiana vizuri na UTT microfinance hivyo wanaweza kukopeshwa na kukuza uzalishaji wa bidhaa ili kwendana na mahitaji ya soko. 
Alisema tufikirie zaidi katika kuuza bidhaa zetu nje ya nchini kwani soko bado ni kubwa tatizo ni uzalishaji na viwango. 
Aliwapongeza kwa kubuni jiko ambalo limekuwa na soko  kubwa hapa nchini na kuwataka waongeze uzalishaji wa majiko hayo na kutoa wito kwa watanzania kupenda kutumia bidhaa zinazozalishwa nchini badala.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Bodi ya Kampuni ya Mikono Cultural Heritage, Bw.Henry Clemens alisema uwepo wa duka hili utasaidia kukuza soko la ndani la bidhaa za kitamaduni zinazozalishwa na wajasiriamaliv nchini. 
“dhana ya serikali ya viwanda itatusaidia kulinda soko la bidhaa za ndani na wajasiriamali kunufaika,” alisema Bw.Clemens

Alisema tunaishukuru Serikali kwa kuwa na dhamira ya dhati ya kukuza viwanda hasa vidogo kwani ndio msingi wa maendeleo ya viwanda, tutajitahidi kuhakikisha bidhaa zetu zinakuwa na ubora na kukidhi ushindano wa soko ndani na nje ya nchi. 
Naye Mkurugenzi wa Shirika la Maonyesho la Dunia kwa upande wa Afrika (World Fair Trade Organisation- AFRICA (WFTO-AFRICA), Bw.Bernard Outah kutoka Kenya alisema uzinduzi wa duka hili ni mwanzo nzuri wa kukuza biashara kwa wajasiriamali toka Tanzania.

“jambo kubwa ni kukuza uzalishaji wa bidhaa zenye viwango vya kimataifa ili ziweze kuuzika katika mataifa mengine” alisema Bw.Outah 
Aliongezea kuwa masoko yapo mengi changamoto ni upatikanaji wa bidhaa bora na kwa idadi kubwa, hivyo tukiweza haya viwanda vyetu vitakuwa na kufanya uchumi wa nchi kukua. 
Robino Ntila ni Msanii - uchoraji na uchapaji alisema kwa uwepo wa duka hili bidhaa zao zitakwenda kuuzika kwa bei halali yenye manufaa kwako kuliko ilivyokuwa zamani kwani wamekuwa wakiranguliwa na wait wa kati. 
Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Bw.Charles Mwijage (katikati) akikata utepe kuashiria uzinduzi wa duka la Mikono Fair trade lililopo jijini Dar es salaam. duka hilo linalomilikiwa na Mikono Cultural Heritage Ltd litakuwa likiuza bidhaa za kitamaduni za wajasiriamali ikiwa ni moja ya njia ya kukuza sekta ya viwanda nchini. kulia ni Mwenyekiti wa Bodi wa kampuni hiyo,Bw.Henry Clemens, wapili kulia ni Mkurugenzi wa  Shirika la Maonyesho Duniani kwa upande wa Afrika (World Fair Trade Organisation- AFRICA (WFTO-AFRICA), Bw.Bernard Outah. kushoto kwake ni Mkurugenizi wa kampuni hiyo Bw.Deo kafwa na wapili kushoto ni Mbunge wa Temeke Bw.Abdala Mtolea.
Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Bw.Charles Mwijage akipokea zawadi ya jiko toka kwa Mwenyekiti wa Bodi wa kampuni ya Mikono Cultural Haeritage,Bw.Henry Clemens mara baada ya kuzindua duka la mikono fair tradelitakalouza bidhaa mbalimbali za kitamaduni za wajasiriamali ikiwa ni moja ya njia ya kukuza sekta ya viwanda nchini. katikati ni Mkurugenzi wa viwanda vidogo na biashara ndogo wa Wizara ya viwanda,biashara na uwekezaji, Dkt. Consolata Ishebabi

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...