Na Anthony John,Globu ya Jamii

Wanafunzi  wa Chuo cha Utumishi wa Umma wametoa msaada wa vifaa mbambali ikiwemo Madaftari, sabuni, na baadhi ya vifaa vya Kufanyia usafi katika Kituo cha Mwana Orphan Centre kilichopo Vingunguti Jijini Dar es salaam.

Akizungumza na Mwandishi wa Blogu hii,Rais wa Serikali ya wanafunzi wa Chuo hicho, Hassan Juma ametoa wito kwa vyuo vingine kutoa msaada kwa watoto wasiojiweza ili waweze kuwasaidia watoto hao.

"Kama sisi tunasoma Chuo cha Utumishi wa umma ni lazima tuijali Jamii inayotuzunguka kwa sababu Sisi ni waudumiaji wa jamii tukaona ni vyema leo hii tutoe msaada katika kituo hiki",amesema Juma.

Pamoja na wanafunzi hao kutoa msaada katika kituo hicho Mwenyekiti msaidizi wa kituo hicho Sada Omary ameomba watu mbali mbali wenye uwezo kujitokeza ilikuwasaidia  watoto hao.

"Unakuta Siku nyingine unaenda stoo kuangalia chakula unakuta gunia moja la chakula na watoto wapo wengi na wanahita kula hivyo nichanagamoto kubwa sana kwetu, tuna waomba watu wenye uwezo watusaidie msaada mbali mbali",amesema Sada.
01.Rais wa Serikali ya wanafunzi wa Chuo cha Utumishi wa Umma-Magogoni, Hassan Juma akikabidhi baadhi ya vifaa kwa Watoto waishio katika mazingira magumu wa kituo cha Mwana Orphan Centre kilichopo Vingunguti jijini Dar es Salaam.
 Mlezi wa Kituo hicho,Sada Omary akizungumza na Wanafunzi wa Chuo cha Utumishi waliotembelea Kituo hicho.
 Picha ya pamoja 

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...