Tunapenda kuwatarifu kwamba kesho jumamosi uwanja wa kinesi, kutakuwa na mpambano wa kirafiki kati ya timu ya Golden bush Fc and Simba sports club katika uwanja wa Kinesi. Golden Bush ni moja ya timu machachari kabisa inayoshiliki ligi daraja la nne wilaya ya Kinondoni, itashuka uwanjani kwa nia ya kuzima kazima tambo za makocha wa Simba inayoongozwa Abdallah king Kibadeni.
Golden Bush tumefanya maandalizi ya kutosha kabisa chini ya Mwalim Katina Shijja, Mkurugenzi wa ufundi bwana Madaraka Seleman “mzee wa Kiminyio” na meneja wa timu bwana Waziri Mahadhi “Mandieta”. Kwakifupi timu yetu iko tayari kukabiliana na Wekundu wa Msimbazi na vijana wako tayari kuonyesha upinzani wa kutosha kabisa.
Imetolewa na Onesmo Waziri
Msemaji wa timu
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...