
Aliyekuwa kocha Simba Patrick Liewig (pichani) amerejea nchini na kuitaka klabu hiyo imlipe malimbikizo ya mshahara wake kisha iachane naye kwa amani.
Simba iliachana na Liewig baada ya kutoridhishwa na matokeo ya mechi za msimu uliopita na kuishia kukamata nafasi tatu.
Akizungumza na Ripota wetu mara baada ya kuwasili jijini Dar es Salaam jana alfajiri,Liewig alisema,hawezi kulazimisha Simba imwongezee mkataba isipokuwa anachohitaji ni malipo ya malimbikizo ya mishahara yake.
"Nimekuja hapa kwaajili ya kutaka kujua kinachoendelea, sababu nimesikia tu juu juu kuwa sitakiwi kwenye timu na sijaambiwa rasmi.
"Pamoja na hayo mimi sina tatizo,kama wameamua hivyo kuachana na mimi sawa isipokuwa wanilipe fedha zangu ninazodai kwani ni haki yangu na ndio maana nimekuja Tanzania"alisema Liewig
Aliongeza" Mkataba wangu umeisha Juni lakini kuna fedha zangu bado nawadai hivyo siwezi kuziacha hivi hivi, lazima wanilipe ndipo tumalizane kwa amani".
Kocha huyo aliichukua Simba mikononi mwa kocha aliyetimuliwa Milovan Cirkovic na alianza kuinoa timu hiyo kwenye mzunguko wa pili wa Ligi Kuu Tanzania Bara.
Kocha huyo alisifika kwa ukali wake kwa wachezaji na hivyo kuamua kufanya uamuzi mgumu wa kuwasimamisha baadhi ya wachezaji nyota wa timu hiyo kwa madai ya utovu wa nidhamu na kuwatumia vijana katika michezo 10.
Hata hivyo habari za ndani zinadai kuwa kocha huyo anaidai klabu hiyo malimbikizi ya mshahara wa miezi mitatu unaofikia kiasi cha dola 36,000.
Kaimu Makamu mwenyekiti wa Simba Joseph Itangare alisema hawana taarifa ya ujio wa kocha huyo lakini wanasubiri kama atawasiliana nao basi watamsikiliza.
"Sisi hatujui kama amefika hapa nchini lakini tunangoja kama atawasiliana na sisi tutafanya mazungumzo naye" alisema.
mishahara hawalipi wanategemea kocha atafundishaje na njaa na mawazo pia kama sio kujitakia
ReplyDeletewao mabosi wanakula na kuiba
wamlipe baba wa watu aondoke, wana tia aibu Tanzania na kufukuza wengine wakitaka kuja nchini kwa chochote.
Mlipeni pesa yake aondoke zake na msijibalaguze eti hamjui kama yupo...mnajua sana acheni dhuluma za wazi, mpeni chake aanze wezi wakubwa nyie
ReplyDeleteMakubwa haya jamani!!!! Mtu anadhulumiwa haki yake hivi hiviiiii bila haya!! Inamaana mpaka leo hii mnataka watu wafanye kazi bila kulipwa? Mnatia aibu kutokumlipa babu wawatu! Mpeni chake asepe wacheni kujifanya machizi. Sasa kapoteza nauli yake kuja kudai hela hapo bado chakula, malazi na usafiri!!! Hakika mnatia aibu sana.
ReplyDeleteMlipeni upesi. Kujua au kutojua kama amekuja haiwaondlei liability ya kumplipa pesa zake za mshahara amazowadai. Yaani mnamfanyisha kazi kocha miezi mitatu bila kumpilipa na bado mnategemea matokeo mazuri kutoka kwakwe? Lo! Mnatia aibu sana.
ReplyDeleteSINA CHA KUONGEZA YOTE YAMESHA SEMWA!!
ReplyDeleteMAMBO MENGINE AIBU.\
MDAU SIMBA - CM