HALI ya msanii wa filamu nchini,Juma Said Kilowoko maarufu kama Sajuki imeelezwa si ya kuridhisha mara baada ya msanii huyo juzi kuanguka jukwaani kwa kuishiwa nguvu wakati alipopanda jukwaani kuwasalimia mashabiki waliofurika kumtizama.
Tukio hilo lilitokea Jumapili katika tamasha la wasanii wa filamu na wale wa muziki wa kizazi kipya lililofanyika ndani ya uwanja wa michezo wa Sheikh Amri Abeid wakati msanii huyo alipopandishwa jukwaani kuwasalimia mashabiki wake.
Mara baada ya msanii huyo kupandishwa jukwaani alipewa kipaza sauti ili aweze kuwasalimia mashabiki wake lakini katika hali ya kawaida alifanikiwa kutamka neno moja tu”ahhh" na kisha kudondoka chini ya jukwaa lakini kabla ya kutua chini alidakwa na wasanii waliokuwa pembeni yake.
Wasanii wenzie walimkalisha chini ya jukwaa hilo ili aweze kupumzika na kisha baada ya muda mfupi walimshusha chini ya jukwaaa hilo ili aweze kupata muda wa kupumzika zaidi.
Akihojiwa muda mfupi mara baada ya kushuka jukwaani Sajuki kwa sauti ya upole alisema kwamba hali yake kiafya si nzuri kwa kuwa hana nguvu na anahitaji matibabu zaidi.
”Kaka hali yangu si nzuri kabisa naumwa sana sijisikii vizuri”alisema Sajuki huku akionekana mnyonge zaidi
Sajuki akipumzika kwa muda baada ya kuanguka
Sajuki akinyanyuliwa
Akitelemshwa toka jukwaani
Pole sana Sajuki Mungu akujalie upone haraka.
ReplyDeleteJipumzikie baba, hujapona bado!!
ReplyDeleteUmeshapona lakini mwili unachukua ukishapata mtikisiko mkubwa unahitaji kupumzika muda mrefu ili urudishie virutubisho mwilini.
ReplyDeleteMungu akutie Nguvu
Hii inaonyesha wazi kuwa kazi ya wasanii si nyepesi kama inavyoonekana machoni.
ReplyDeleteA man will die doing what he loves to do i.e., either worshiping the creator or disobeying him through smoking, drinking, Fornicating and the list continue on and on. This guy should think about himself and what comes next. This is my humble advise to all you young people there trying to dwell in materialistic world of today, because a day is coming soon when the earth will be shaken to the extent a mother will drop her baby, a young boy’s hair will become grey due to the fear of the day and people will be questioned on what they used to do.
ReplyDeleteAfya yako haijatengemaa vizuri na hapo hapo unataka kuendekeza usanii, jiangalie afya yako! Unafikiri dawa ni chumvi? Umeuguwa muda mrefu na unapaswa upumzike ili mwili urudishe nguvu! Matatizo mengine ya kujitakia
ReplyDeleteTHANK YOU SO MUCH Anonymous Tue Dec 18, 11:27:00 PM 2012 tunaomba uelimishe jamii kila siku kwa neno na utumie muda wako kutoa comment/mada ktk blogu yetu hii muhimu.
ReplyDeleteKAKA POLE SANA,ANGALIA AFYA YAKO NA PIA KUMBUKA SIKU ZOTE KIKULACHO KII NGUONI MWAKO,USIWAAMINI MARAFIKI SANA,KAKA HANGAIKA KIDOGO UTAKUWA FITI ASANTE.MDAU WALTHAMSTOW.
ReplyDeleteWadau naona kama hapa tumeachwa nyuma kidogo Sajuki alikuwa Arusha kufanya tamasha ili apate pesa za kujitibu ana tatizo kubwa pengine kuliko lile la mwanzo ni vile ile radio iliyomsapoti mwanzo haijamualika aliongelee na ndio maana wengi hawajui kwanini alipanda jukwaani Arusha. ana kansa ya mgongo
ReplyDeleteMungu ni mwema na atakuwezesha Sajuki. Usikate tamaa na mzidi kumuomba kwani hiyo ni mitiani tu wastara nyie zidini kuomba na kuwa na moyo dhabiti
ReplyDeleteWenu,
Magreriq