HALI ya msanii wa filamu nchini,Juma Said Kilowoko maarufu kama Sajuki imeelezwa si ya kuridhisha mara baada ya msanii huyo juzi kuanguka jukwaani kwa  kuishiwa nguvu wakati alipopanda jukwaani  kuwasalimia mashabiki waliofurika kumtizama. 

 Tukio hilo lilitokea Jumapili katika tamasha la wasanii wa filamu na wale wa muziki wa kizazi kipya lililofanyika ndani ya uwanja wa michezo wa Sheikh Amri Abeid wakati msanii huyo alipopandishwa jukwaani kuwasalimia mashabiki wake.

 Mara baada ya msanii huyo kupandishwa jukwaani alipewa kipaza sauti ili aweze kuwasalimia mashabiki wake lakini katika hali ya kawaida alifanikiwa kutamka neno moja tu”ahhh" na kisha kudondoka chini ya jukwaa lakini kabla ya kutua chini alidakwa na wasanii waliokuwa pembeni yake. 

Wasanii wenzie walimkalisha chini ya jukwaa hilo ili aweze kupumzika na kisha baada ya muda mfupi walimshusha chini ya jukwaaa hilo ili aweze kupata muda wa kupumzika zaidi. 

 Akihojiwa  muda mfupi mara baada ya kushuka jukwaani Sajuki kwa sauti ya upole alisema kwamba hali yake kiafya si nzuri kwa kuwa hana nguvu na anahitaji matibabu zaidi. ”Kaka hali yangu si nzuri kabisa naumwa sana sijisikii vizuri”alisema Sajuki huku akionekana mnyonge zaidi
Sajuki akipumzika kwa muda baada ya kuanguka
Sajuki akinyanyuliwa
Akitelemshwa toka jukwaani

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 10 mpaka sasa

  1. Pole sana Sajuki Mungu akujalie upone haraka.

    ReplyDelete
  2. Jipumzikie baba, hujapona bado!!

    ReplyDelete
  3. Umeshapona lakini mwili unachukua ukishapata mtikisiko mkubwa unahitaji kupumzika muda mrefu ili urudishie virutubisho mwilini.

    Mungu akutie Nguvu

    ReplyDelete
  4. Hii inaonyesha wazi kuwa kazi ya wasanii si nyepesi kama inavyoonekana machoni.

    ReplyDelete
  5. A man will die doing what he loves to do i.e., either worshiping the creator or disobeying him through smoking, drinking, Fornicating and the list continue on and on. This guy should think about himself and what comes next. This is my humble advise to all you young people there trying to dwell in materialistic world of today, because a day is coming soon when the earth will be shaken to the extent a mother will drop her baby, a young boy’s hair will become grey due to the fear of the day and people will be questioned on what they used to do.

    ReplyDelete
  6. Afya yako haijatengemaa vizuri na hapo hapo unataka kuendekeza usanii, jiangalie afya yako! Unafikiri dawa ni chumvi? Umeuguwa muda mrefu na unapaswa upumzike ili mwili urudishe nguvu! Matatizo mengine ya kujitakia

    ReplyDelete
  7. THANK YOU SO MUCH Anonymous Tue Dec 18, 11:27:00 PM 2012 tunaomba uelimishe jamii kila siku kwa neno na utumie muda wako kutoa comment/mada ktk blogu yetu hii muhimu.

    ReplyDelete
  8. KAKA POLE SANA,ANGALIA AFYA YAKO NA PIA KUMBUKA SIKU ZOTE KIKULACHO KII NGUONI MWAKO,USIWAAMINI MARAFIKI SANA,KAKA HANGAIKA KIDOGO UTAKUWA FITI ASANTE.MDAU WALTHAMSTOW.

    ReplyDelete
  9. Wadau naona kama hapa tumeachwa nyuma kidogo Sajuki alikuwa Arusha kufanya tamasha ili apate pesa za kujitibu ana tatizo kubwa pengine kuliko lile la mwanzo ni vile ile radio iliyomsapoti mwanzo haijamualika aliongelee na ndio maana wengi hawajui kwanini alipanda jukwaani Arusha. ana kansa ya mgongo

    ReplyDelete
  10. Mungu ni mwema na atakuwezesha Sajuki. Usikate tamaa na mzidi kumuomba kwani hiyo ni mitiani tu wastara nyie zidini kuomba na kuwa na moyo dhabiti
    Wenu,
    Magreriq

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...